Home KITAIFA SERIKALI IMEFANIKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI-DK.MWINYI

SERIKALI IMEFANIKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI-DK.MWINYI

Na Mwandishi wetu, Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imefanikiwa sana kuongeza ukaribu na wananchi kwa kusikiliza changamoto na kuzitatua kwa haraka kupitia Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi (SNR).

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo katika hafla ya Maadhimisho ya Miaka 3 ya Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi(SNR) Machi 16, 2024 katika Viwanja vya Ikulu Mnazi Mmoja.

Amesema Mfumo wa SNR ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wananchi pia ni kigezo cha utawala bora unaozingatia ushirikishwaji wa wananchi.

“Kitengo cha SNR kina wajibu kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kutumia njia mbalimbali kwa wananchi ili waweze kutumia vema Mfumo huu kwa madhumuni yaliyokusudiwa,” amesema Dk.Mwinyi.

Aidha Dk.Mwinyi amesema katika kipindi cha Miaka 3 tangu kuanzishwa kwa Mfumo wa SNR jumla la malalamiko 13,517 yamepokelewa kati ya hayo 11,116 yamepatiwa ufumbuzi na 2,351 yanaendelea kufanyiwa kazi katika hatua mbalimbali.

Viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyombo vya ulinzi na usalama na Vyama vya Siasa wamehudhuria hafla hiyo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here