


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 30, 2024 amesafiri kwa kutumia Usafiri wa treni ya Mwendo Kasi (SGR) kutokea Dodoma kwenda Dar es Salaam ambako atakuwa mgeni rasmi katika Mkutano wa 12 wa Shirikisho la Watoa Huduma za Afya Afrika Mashariki utakao fanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).