Home KIMATAIFA DK.BITEKO AWASILI NCHINI KENYA KWA ZIARA YA KIKAZI

DK.BITEKO AWASILI NCHINI KENYA KWA ZIARA YA KIKAZI

Kenya

NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko leo amewasili jijini Nairobi nchini Kenya kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Pili wa Masuala ya Nishati ya Nyuklia kati ya Marekani na nchi za Afrika ( US-Africa Nuclear Energy  Summit).

Mkutano huo wa masuala ya Nyuklia  utahusisha mijadala kuhusu utayari wa Sekta ya Nishati katika kusimamia mnyororo wa thamani kwa ajili ya uendelezaji wa nyuklia pamoja na umuhimu wa kuwashirikisha wanawake na vijana katika Sekta

Katika ziara hiyo, Dk. Biteko ameambatana na Watendaji kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here