Home KITAIFA DK. BITEKO AWATAKA WAZAZI KUPELEKA WATOTO SHULE

DK. BITEKO AWATAKA WAZAZI KUPELEKA WATOTO SHULE

๐Ÿ“Œ Asisitiza nia yake kuchochea maendeleo Bukombe

๐Ÿ“Œ Ataka ufuatiliaji wa wasioenda shule ufanyike hadi ngazi ya kaya

๐Ÿ“Œ Daraja la mpakani kati ya Burenga na Mbogo kuanza kujengwa

Geita

NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Dk. Doto Biteko amewahimiza wazazi na walezi kuhakikisha watoto wao wanapata elimu kwa kuwa ndio nguzo ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Amesema hayo Juni 7, 2024 wakati akihutubia mkutano wa wananchi katika Shule ya Msingi Bufanka iliyopo Kijiji cha Bufanka, Kata ya Bugelenga, Jimbo la Bukombe mkoani Geita.

โ€œ Naona aibu kuona watoto wanazuiwa wasiende shule, niwaombe wazazi tupeleke watoto shule. Wenyeviti wa Vijiji niwaombe kama kuna mtoto kwenye kijiji chako ambaye anatakiwa kwenda shule na haendi, nenda kwenye kaya hiyo kuwaeleza kuhusu umuhimu wa elimu ili mtoto huyo aweze kwenda shuleโ€, amesisitiza Dk. Biteko.

Amesema Serikali imeendelea kujenga shule ambapo kwa sasa Wilaya ya Bukombe ina shule za sekondari 7 na shule 5 za kidato cha tano na sita ambapo awali kulikuwa na shule moja.

Katika kutilia mkazo umuhimu wa elimu, Dk. Biteko amechangia ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa ya shule iliyopo katika Kata ya Bugelenga kwa kutoa mabati 135 na mifuko 400 ya saruji kwa ajili ya ukamilishaji wa miradi mbalimbali.

Amewataka wananchi wa Kijiji cha Bufanka na Jimbo la Bukombe kwa ujumla kujiandaa kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwaka huu kwa kuchagua viongozi wenye sifa watakaosaidia kuleta maendeleo.

โ€œViongozi wa Chama chetu na Katibu Kata anzeni kwenda kwenye kata zetu kuwaambia mabalozi tukutane ili tujadiliane kuhusu uchaguzi, watu wengine wanashangaa Chama Cha Mapinduzi kinashindaje, wajue tu ni kwa kuwa tunajipanga mapema kwa ajili ya kesho,” amesema Dk. Biteko.

โ€œ Tujue watu wangapi wanapiga kura na nani anataka kugombea lakini niwaambie tu tusikubali kutumia rushwa, tuvipinge vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi. Viongozi wa Kata na Shina andaeni viongozi vizuri wenye sifa za kuchaguliwa ambao watasaidia kuleta maendeleo, tunataka wilaya yetu iwe mahali salama pa kuishi kwa kuchagua watu wenye maono au mawazo mazuri yatakayosaidia utatuzi wa changamoto sio kuchagua mtu ilimradi tu ana fedhaโ€, amefafanua na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni humo.

Katika hatua nyingine, Dk. Biteko amesema kuwa, Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan atafanya ziara mkoani Geita na kwa Wilaya ya Bukombe miradi mingi itaendelea kutekelezwa na kwamba miradi iliyotekelezwa ni sehemu tu hivyo yeye kama Mbunge ataendelea kuhakikisha maendeleo ya kweli yanaenda kwenye maeneo ya wananchi.

Naye, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Festo Dugange amesema kuwa Dk. Biteko amesemea miradi mingi kwa ajili ya kuwasaidia wananchi na Mhe. Rais Samia ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya na zahanati.

โ€œ Hapo awali huduma zilikuwa mbali na gharama za kwenda kupata matibabu zilikuwa juu kakini Mhe. Dkt. Biteko aliona changamoto hiyo na alipomueleza Mhe. Rais Samia Wilaya hii ilipewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo,โ€ amesema Dugange.

Ameongeza kuwa Jimbo hilo pia limepata zaidi ya shilingi milioni 900 kwa ajili ya sekta ya afya na Kata ya Bugelenga peke yake wamepata shilingi milioni 50 na maeneo mengine tayari wamepata fedha na zahanati zimejengwa.

Pia, Rais ameelekeza shilingi milioni 500 nyingine kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Bukombe ambapo itajengwa hospitali ya watoto njiti.

Akizungumzia daraja lililopo mpakani kati ya Bugelenga na Mbogo, Dugange amesema โ€œ Serikali tayari imetenga shilingi milioni 585 kwa ajili ya ujenzi wa daraja, na shilingi milioni 85 zimeshaletwa hapa, TARURA wataanza kutafuta mkandarasi na katika kipindi cha ndani ya mwezi mmoja na nusu ujenzi wa daraja hili utaanza na baadaye tutaanza ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 30,โ€

Kuhusu sekta ya elimu, amesema kuwa ndani ya kipindi cha miaka minne Jimbo hilo limepata zaidi ya shilingi bilioni 9 kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa shule za msingi na sekondari.

Aidha, amewapongeza wananchi kwa kuwa na mbunge hodari, mchapakazi na mwenye kujali na kutatua changamoto zao.

Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Geita, Nicholaus Kasendamila amemshukuru Dk. Biteko kwa kuendelea kuwasaidia wananchi wa Bukombe kwa kuhakikisha wanapata maendeleo kwa kuwa na miradi mbalimbali ikiwemo ya shule, hospitali na barabara.

Aidha, amewasihi wananchi wa Bukombe kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa โ€œHuu ni mwaka wa uchaguzi tunatakiwa kujiandaa na viongozi wa CCM katika Mkoa huo tuhamasishe wapiga kura kushiriki katika uchaguzi na hatimaye kuchagua viongozi wazuri,โ€amesema

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Geita, Rose Busiga amesema kuwa Mbunge wa Jimbo hilo Dk. Biteko ameendelea kutatua changamoto zao mbalimbali ikiwemo ya mawasiliano na tayari fedha za kujenga minara 9 ya mawasiliano zimeshaletwa jimboni.

Aidha, pamoja na mkutano huo wa hadhara wananchi wamepata fursa ya kuchangia damu, kupima afya pamoja na kupata elimu ya masuala ya lishe.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here