Home KITAIFA VIJIJI 31 KATI YA 34 MBULU MJINI VYAPATIWA UMEME

VIJIJI 31 KATI YA 34 MBULU MJINI VYAPATIWA UMEME

Dodoma

NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Jimbo la Mbulu Mjini lina Vijiji 34 ambapo Vijiji 31 kati ya hivyo vimepata umeme.

Ameeleza hayo Juni ,7 2024 bungeni jijini Dodoma ambapo amesema uwa kwa Vijiji vilivyosalia utekelezaji wa miradi unaendelea na kazi itakamilika Juni, 2024.

Ameongeza kuwa, Jimbo la Mbulu Mjini lina mitaa 58 ambapo mitaa 46 ina umeme na mitaa 12 ambayo imesalia itapatiwa umeme kupitia mradi wa kupeleka umeme vitongojini ambao utaanza mwaka wa fedha 2024/2025.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here