Home KITAIFA USAFIRI WA ANGA NI KICHOCHEO CHA UKUAJI UCHUMI-DK.MWINYI

USAFIRI WA ANGA NI KICHOCHEO CHA UKUAJI UCHUMI-DK.MWINYI

Na Mwandishi wetu, Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema sekta ya utalii ina mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi wa nchi kupitia usafiri wa anga ambao ni kichochea kikuu cha ukuaji wa uchumi.

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipofungua Kongamano la sita la usafiri wa anga Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Hoteli ya Verde Mtoni, Mkoa wa Mjini Magharibi Mei,15 2024.

A Rais Dk.Mwinyi ameeleza hatua iliyofikiwa na SMZ katika ukuaji wa sekta ya usafiri wa anga ya kutekeleza miradi kwa kukamilisha jengo la abiria uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume Terminal 3, kuanza ujenzi jengo jipya la abiria Terminal 2 litakalohudumia abiria zaidi 1,300,000 kwa mwaka, ujenzi na ukarabati wa ujenzi wa jengo la zamani la Terminal 1, ujenzi wa jengo la biashara na ofisi katika jengo la tatu la abiria, jengo la kuhifadhi na kusafirisha hasa chakula vinavyoharibika kwa haraka, ujenzi wa vituo vitatu vya huduma za mafuta ya ndege, ujenzi wa uwanja wa ndege na upanuzi wa kiwanja cha ndege Pemba na jengo jipya la abiria na uwanja wa ujenzi wa kiwanja cha Nungwi.

Aidha amewahimiza washiriki wote wa kongamano hilo kujadili na kutoa mapendekezo kwa kubainisha fursa zitazoweza kutumika katika sekta ya usafiri wa anga kwa manufaa ya Nchi wanachama wa Jumuiya ya Mashariki .

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here