Home KITAIFA WAZIRI MKUU ANATARAJIA KUWA MGENI RASMI TULIQ MARATHON

WAZIRI MKUU ANATARAJIA KUWA MGENI RASMI TULIQ MARATHON

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 10, 2024 amewasili uwanja wa ndege wa Songwe ambapo kesho Mei 11, 2024 atakuwa mgeni rasmi katika mbio za Mbeya Tulia Marathon 2024.

Akiwa mkoani Mbeya, Waziri Mkuu atakagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi.

Pichani, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera, Viongozi wa vyama vya siasa na Serikali, viongozi wa dini na mila.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here