Home KITAIFA MAJALIWA AKUTANA MWANA WA MFALME, ZAHRA AGA KHAN

MAJALIWA AKUTANA MWANA WA MFALME, ZAHRA AGA KHAN

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Mei 3, 2024 amekutana na Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Taasisi ya Huduma za Aga Khan, Mwana wa Mfalme, Zahra Aga Khan na ujumbe wake, ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amemwambia Kiongozi huyo kuwa Serikali inatambua jitihada kubwa zinazofanywa na Taasisi hiyo hasa katika sekta ya afya na elimu na amemuahidi kuwa serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za uwekezaji zinazofanywa na taasisi ya hiyo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here