Home KITAIFA MAJALIWA SIKU YA MEI MOSI WAFANYAKAZI KUTAFAKARI NA KUTATHIMINI MALENGO WALIOJIWEKEA

MAJALIWA SIKU YA MEI MOSI WAFANYAKAZI KUTAFAKARI NA KUTATHIMINI MALENGO WALIOJIWEKEA

Na Mwandishi wetu, Arusha

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI MOSI) ambayo huadhimishwa kila mwaka ni siku maalum kwa ajili ya wafanyakazi kutafakari na kutathmini namna walivyotekeleza malengo waliyojiwekea katika mwaka husika.

Amesema hayo leo Mei Mosi, 2024 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani inayofanyika kitaifa mkoani Arusha, kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo ni Makamu wa Rais, Dk. Philip Isdor Mpango ambaye amemwakilisha Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuwa siku hiyo inatoa fursa kwa wafanyakazi wote duniani kuweka mipango kwa ajili ya mwaka unaofuata na ndiyo maana inafanyika kipindi ambacho nchini nyingi duniani zinakuwa katika maandalizi ya Bajeti.

“siku hii ni muhimu sana na inatukumbusha wajibu wetu wafanyakazi wa kujadiliana kwa pamoja changamoto zilizopo katika utendaji wetu wa kazi na kuzitafutia ufumbuzi kwa pamoja na hatimaye kuleta tija katika maeneo ya kazi,”amesema Majaliwa


Amewapongeza watumishi wote kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuwaletea watanzania maendeleo.

“Sisi sote ni mashahidi wa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitatu kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia na kijamii,”amesema

Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ni “Nyongeza ya Mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha”

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here