Home KITAIFA RAIS DK.MWINYI AZINDUA TAASISI YA WASANIFU NA WAHANDISI ZANZIBAR

RAIS DK.MWINYI AZINDUA TAASISI YA WASANIFU NA WAHANDISI ZANZIBAR

Na Mwandishi wetu, Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo unazingatia dhana ya ushirikishwaji wa Wahandisi wa kitanzania kupitia miradi endelevu ya kimkakati ya uwekezaji nchini.

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipozindua Taasisi ya Wasanifu , Wahandisi na Wakadiriaji Zanzibar na Mkutano mkuu wa mwaka huu katika ukumbi wa Hoteli ya Verde, Mkoa wa Mjini Magharibi Aprili, 20 2024.

Amesema Serikali zote mbili ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinafanya jitihada ikiwemo kuweka mazingira wezeshi kujiajiri, kuhamasisha utambuzi wa fursa mbalimbali, kurejesha stadi za ujuzi, elimu ya uanagenzi vyuoni pamoja na kutenga bajeti kwa ajili utafiti na ubunifu mbalimbali.

Ameeleza kuwa serikali kwa upande wake kupitia Uchumi wa Buluu imeendeleza sera ya kuajiri wasanifu, wahandisi na wakadiriaji wazalendo.

” Serikali inathamini mchango wa fani mbalimbali katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ikiwemo miradi ya ujenzi,” Dk. Mwinyi.

Amewapongeza wakandarasi na washauri wazawa kwa kufanya kazi za uhandisi kwa ufanisi katika miradi mbalimbali waliyotekeleza.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here