Home KITAIFA WAANDISHI WA HABARI WAPEWA ELIMU KUHUSU RIBA YA BENKI KUU...

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA ELIMU KUHUSU RIBA YA BENKI KUU (CRB).

Na Mwandishi wetu@Lajiji Digital 

MKURUGENZI wa  Utafiti na Sera za Uchumi  wa Benki Kuu  ya Tanzania (BoT),Dk.  Suleiman Missango  amesema kuwa Riba ya Benki Kuu (CRB) hutolewa kama Riba elekezi kwa mabenki  kuweza kukopa fedha kutoka  Benki Kuu. 

Pia amefafanua sababu  ya ongezeko la Riba ya Benki Kuu  kuwa asilimia sita kuwa ni kudhibiti mfumuko wa bei  siku za usoni.

Hayo ameyabainisha Leo prili 8 2024 jijini Dar es Salaam baada  ya kukutana na waandishi wa habari  wa vyombo tofauti  Dk.  Missango  ili kutoa elimu kuhusiana na mfumo mpya wa sera ya fedha  unatumia Riba ya Benki Kuu (CRB).

Amesema Benki Kuu imekuwa ikifanya kazi  kwa karibu na mabenki  ili kudhibiti ujazi wa fedha katika mabenki nkwenye mzunguko.

“Mfumo wa sera ya fedha unaotumia Riba ya Benki Kuu  utasaidia mabenki na taasisi nyingine za fedha  kupanga viwango  vyao vya Riba  na sio kuweka ukomo wa riba kwa mabenki  na taasisi zinazotoa mkopo,”amesema Dk. Missango. 

Amesema  mwenendo wa uchumi wa dunia ulikuwa unaashiria  uwepo wa mfumuko wa bei hivyo ikaona iongeze riba  kutoka asilimia 5.5 hadi asilimia sita katika robo ya pili  kuanzia Aprili mwaka huu.

Amesema kupanda kwa riba hiyo kumezingatia  ukuaji wa uchumi kwa maana ya uwepo wa fedha za kutosha  katika mzunguko kulingana na malengo yaliyowekwa.

“Wengi walijua tunakwenda kuweka  ukomo wa riba sio kweli, kwa kupandisha riba hiyo  maana yake tunapunguza ukwasi  katika  mzunguko na hivyo  kudhibiti  mfumuko wa bei  kwa siku zijazo.

 “Kupanda  kwa riba hiyo kumezingatia ukuaji wa uchumi , maamuzi mengine  yatachukuliwa  Julai mwanzoni na riba hii ni ya robo  ya kwanza ya Aprili, mwaka huu  na inaweza kupungua au kuongezeka  kwa kadri ya uchambuzi  utakavyokuwa,” amesema Dk.Missango

Ameongeza kuwa tangu Benki Kuu  ianzishe  mfumo wa riba  ya Benki Kuu mwaka  huu badala ya mfumo wa zamani wa ujazi wa fedha hali imeendelea kuwa tulivu na mapokeo yamekuwa mazuri kwa wadau.

Ameeleza kuwa hali hiyo imetokana na juhudu kubwa ya kutoa elimu  kwa wadau katika sekta  na imeahidi kuendelea  kutoa elimu kwa wanananchi kuweza kufanya uamuzi sahihi katika shughuli za kiuchumi.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here