Home AFYA Kampuni ya Vertex Group Kuunga mkono juhudi za Rais Dk.samia kwa...

Kampuni ya Vertex Group Kuunga mkono juhudi za Rais Dk.samia kwa kutangaza Tiba utalii

Na Mwandishi wetu 

KAMPUNI ya  Vertex Group Experts imesema inamuunga mkono juhudi za Rais Dk.samia Suluhu Hassan kwa kutangaza nchi za jirani na Afrika katikaTiba Utalii  ili waweze kuwafikia wagonjwa  wengi na kuongeza Pato la Taifa. 

Akizungumza leo Machi 4 jijini Dar es Salaam na waandishi wa  habari Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo, Herbert  Swai amesema lengo  la Kampuni  ni kutoa huduma za Tiba Utalii kwa kuwaunganisha wagonjwa  hospitali nchini na kurahisisha urahisi wa kupata. 

Amesema Kampuni hiyo  tangu kuanzishwa ina muda wa miaka miwili  ikiwa mikakati yao ni kuendelea kukuza Tiba utalii  na kuweza zaidi ili  wagonjwa wanaokuja kutibiwa na  kutangaza nchi  kutokana na huduma nzuri walizopata.

“Tunataka kuondoa dhana iliyojengeka kwa watu kuwa kutibiwa Hospitali ya Taifa Mhimbili ni gharama kubwa hapana  tuta hakikisha wagonjwa wa nje na wandani wanapata huduma bora na kwa gharama nafuu na kwaharaka,”amesema Swai.

Amesema Rais Dk. Samia  katambulisha Tanzania katika Afrika Mashariki ni kitovu cha huduma bora za afya lazima wafanyekazi ya kutoa huduma bora kwa wagonjwa wa nje wanaokuja kutibiwa nchini. 

Swai amesema Kampuni hiyo  kwa takwimu za mwaka 2023 walipokea wagonjwa 47 kutoka nchi mbalimbali walitibiwa nchini katika Hospitali ya Mhimbili  na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).

Aidha amesema kwa sasa wanakabiliwa na changamoto ya wagonjwa wanakuja kutibiwa  wengine wanakuwa hawajui lugha,  Kiswahili  wala kingereza wanaongea lugha zao hivyo wanawakalimani kwaajili ya  wagonjwa wa nje ya nchi. 

Ameongeza kuwa  Tiba utalii  inawahusu watanzania wote na Kampuni hiyo ipo kwaajili ya kuwahudumia na kuwasiidia kupata huduma kwa haraka na ipo kisheria na inatambulika.

Akizungumza baadhi ya wagonjwa kutoka Visiwa vya Comoro waliopata huduma ya kutibiwa kupitia Kampuni hiyo, Mohamed Abdulla amesema wanaishukuru Kampuni  hiyo imewawezesha kupata huduma katika Hospitali ya Taifa Mhimbili na wanaendelea vizuri. 

“Tunaahaidi kuwa mabalozi wazuri na kuwashauri wananchi wa Visiwa vya Comoro kuja kutibiwa Tanzania kwasababu kuna huduma nzuri  kama hauna ndugu wa kukusaidia kuna Kampuni ambayo inasimamia kuanzia matibabu yako hadi mwisho,”amesema Abdalla.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here